Friday, July 29, 2011

maadhimisho ya miaka 50 ya uanzishwaji wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere

Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere , Kivukoni na Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salimu akizindua maadhimisho ya miaka 50 ya Chuo hicho leo jijini Dar es salaam. Chuo hicho kimeanzishwa tarehe 29 Julai mwaka 1961.Wageni wengine ni pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba .
Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba akitoa mada juu ya mchango wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere katika maendeleo ya Taifa leo jijini Dar es salaam wakati wa uzindua maadhimisho ya miaka 50 ya Chuo hicho . Chuo hicho kianzishwa tarehe 29 Julai mwaka 1961.
Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere , Kivukoni Dkt John Magotti akitoa hotuba ya ukaribisho leo jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 50 ya uanzishwaji wa Chuo hicho.
Wanajumuiya wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere , Kivukoni wakicheza muziki leo jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 50 ya Chuo hicho .
Wanajumuiya wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere , Kivukoni wakimsikiliza kwa makini hotuba ya uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 50 ya Chuo hicho iliyotolewa leo jijini Dar es salaam na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho na Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim(hayupo pichani).
Picha na Tiganya Vincent- MAELEZO- Dar es salaam.

No comments: