Monday, July 25, 2011

SAKATA LA KUJIVUA GAMBA: WENYEVITI MIKOA WALIPINGA, BARAZA KUU UVCCM LAUNGA MKONO ZIARA ZA KINA NAPE

Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Benno Malisa
---------- ---
MPANGO mkakati wa kujivua gamba kwa lengo la kurejesha uhai ndani ya CCM unaelekea kuwa bomu la maangamizo kwa chama hicho, baada ya baadhi ya wenyeviti wa mikoa kuupinga huku wakiagiza wafuasi wao kuwashusha majukwaani makada wanaoupigia debe.Wakati wenyeviti hao wakiupinga, Baraza Kuu la Umoja wa Vijana CCM (UVCCM), jana limetoa tamko rasmi la kuunga mkono ziara hizo zinazofanywa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa chama hicho, Nape Nnauye za kutekeleza mkakati huo.
Mpango huo wa kujivua gamba ulitangazwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete katika maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa chama hicho kikongwe barani Afrika, lakini jana baadhi ya wenyeviti wake wa mikoa akiwamo, John Guninita wa Dar es Salaam na Hamis Mgeja wa Shinyanga, waliupinga wakisema unamwaga sumu kali dhidi ya chama.


Msimamo wa UVCCM


Baraza Kuu la UVCCM limetoa msimamo wake kuunga mkono ziara za mikoani zinazoongozwa na Nnauye za kujivua gamba huku likiweka bayana kuwa huo ni msimamo wa Halmashauri Kuu (Nec) ya chama na si wa Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi.Kwa Habari Zaidi
Mbali na Nape, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka wamekuwa wakifanya ziara mikoani hasa katika mwisho wa wiki ambazo pamoja na mambo mengine, wamekuwa wakifanya mikutano ya kukipa uhai chama huku wakitangaza uvuaji gamba.



Kaimu Mwenyekiti wa UVCCM, Benno Malisa alisema UVCCM ilipongeza uamuzi wote wa NEC: "Kila kinachofanyika ni sahihi na sisi tunaunga mkono kabisa."


Guninita awatangazia vita
Wakati vijana wakiuunga mkono ziara hizo, juzi Guninita aliwaambia wanaCCM wa Tawi la Sinza kwamba watakapomuona kiongozi yeyote mkubwa wa chama hicho anakikiponda katika wasisite kumshusha jukwaani.
Guninita alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na wanachama hao kuhusu matatizo mbalimbali ya chama hicho na kusisitiza kwamba Waziri Sitta asipojibiwa kauli zake atajiona kuwa ni mkubwa zaidi.
Wiki iliyopita Mwenyekiti huyo alimtupia kijembe Sitta akidai kwamba waziri huyo ana mpango wa kuhakikisha kuwa Serikali ya chama hicho inaondolewa madarakani kwa kuwa bado ana hasira za kupoteza wadhifa wa Spika wa Bunge.
“Chama chetu kinazidi kupoteza sifa, hii ndiyo sababu ya mimi kufanya ziara katika majimbo ambayo yalishindwa katika ngazi zote kukipatia chama ushindi wakati wa uchaguzi. Kumekuwa na viongozi wakubwa wa chama hicho wanaozunguka nchi nzima na kuchochea ili Serikali iondolewe madarakani, nawaambieni mkiwaona viongozi hao wanakiponda chama washusheni majukwaani, wanataka kujiona wao ndiyo wakubwa zaidi ya wengine.”
Alisema chama hicho kinajipanga kikamilifu ili kuhakikisha uchaguziwa mwaka 2015, kinashinda kwa kishindo ikiwa ni pamoja na kupambana na tatizo la rushwa lililokitawala.
Guninita ambaye amekuwa akipingana hadharani na wapambanaji hao wa ufisadi ndani ya CCM, alisema katika uchaguzi huo hawatahitaji ushahidi kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (Takukuru) na kuwa mtu atakapobainika anajihusisha na rushwa atachukuliwa hatua hapohapo.
“Tatizo la rushwa katika chama lipo hasa wakati wa uchaguzi. Ninachotaka kuwahakikishia ni kwamba tunajipanga na katika uchaguzi ujao hatutahitaji ushahidi wa PCCB (Takukuru), tutakapombaini mtu tutampeleka mahakamani wenyewe. Hatutaki aibu ya mwaka huu itukumbe tena.”
Alisema tayari chama kimewabainisha viongozi wote walioingia madarakani kwa rushwa na kuwa wanaendelea kujadiliana hatua za kinidhamu dhidi yao.
Guninita alisema katika uchaguzi wa mwaka 2015, chama hicho hakitapeleka majina ya watu watakaobainika kutoa rushwa kwa ngazi za juu ili wakubalike katika kura za maoni.

Mgeja atoa tahadhari

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja alisema juzi kwamba licha ya kuwakaribisha wapambanaji hao na mkakatio wao wa kujivua gamba katika mkoa wake, waende na majibu ya kero za wananchi.


Alisema viongozi wa chama chake wanatakiwa kwenda na majibu ya kero zilizopo katika mkoa huo za wakulima kuuziwa dawa feki za pembejeo, rushwa, umasikini na rasilimali kama madini kushindwa kuwanufaisha, badala ya kutumia ziara hiyo kuwapaka matope wenzao.


“Ziara za kusafisha chama siyo mbaya, kama zitatumika vyema, lakini hali ambayo imeanza kujitokeza ni wazi haijengi chama, bali inaendelea kumwaga sumu,” alisema.
Endelea>>>








No comments: