Monday, August 15, 2011

VIINGILIO MECHI YA NGAO YA JAMII KATI YA YANGA NA SIMBA VYATAJWA LEO

Viingilio katika mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kufungua msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom kati ya mabingwa watetezi Yanga na Makamu Bingwa Simba itakayochezwa Agosti 17 mwaka huu kuanzia saa 2.00 usiku kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni kama ifuatavyo;

Viti vya bluu sh. 5,000,
viti vya kijani sh. 7,000,
viti vya rangi ya chungwa sh. 10,000,
VIP C sh. 20,000,
VIP B sh. 25,000
na
VIP A sh. 50,000.

Tiketi zimeanza kuuzwa leo mchana (Agosti 15 mwaka huu) kwenye vituo vyote vya mafuta vya Big Bon jijini Dar es Salaam. Pia zinauzwa katika baadhi ya vituo vya OilCom na TSN.

No comments: