Thursday, August 25, 2011

Vodacom Miss Tanzania 2011 wapewa semina kuhusiana na huduma ya M Pesa


Meneja Huduma wa Bidhaa za Vodacom, Elihuruma Ngowi akifafanua jambo juu ya huduma ya M Pesa kwa washiriki wa Shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011 katika kambi yao iliyopo jumba la Vodacom jijini Dar es Salaam leo.
Afisa Utawala wa Huduma ya M Pesa kutoka Vodacom, Emmanuel Pallangyo akigawa viperushi vilivyo na maelezo ya namna huduma ya M Pesa kwa washiriki wa Shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011 katika kambi yao iliyopo jumba la Vodacom jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya washiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakipiga picha na mabaunsa waliovalia vazi la M Pesa “Super Man” baada ya warembo hao na wenzao kupata semina juu ya faida na umuhimu wa kuwa umejisajili katika huduma ya M Pesa leo wakiwa Kambini katika Jumba la Vodacom.
Baadhi ya washiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakijisajili katika huduma ya M Pesa baada ya kupata semina juu ya faida na umuhimu wa kuwa umejisajili katika huduma hiyo jana wakiwa Kambini katika Jumba la Vodacom.
Washiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakipiga picha na mabaunsa waliovalia vazi la M Pesa “Super Man” baada ya warembo hao na wenzao kupata semina juu ya faida na umuhimu wa kuwa umejisajili katika huduma ya M Pesa leo wakiwa Kambini katika Jumba la Vodacom.

No comments: