Kilimo cha chai Njombe
Ujenzi wa kituo cha Afya
Ujenzi wa zahanati.
Mabweni ya wanafunzi.
Jamii maskini kwa kawaida huwa na vipaumbele vingi. Matokeo yake ni kushindwa kuvitekeleza. Wananchi wa mkoa mpya wa Njombe ambao ni wachapa kazi kweli kweli wameikataa falsafa hiyo na wamejiwekea vipaumbele vichache na vya uhakika ili kuujenga mkoa wao. Vipaumbe vya wananjombe ni:
1. Elimu- Kwa kujitolea wananchi wa vijiji na kata za Katulila, Madobole, Miva, Lusitu, Mtila, Mbega, Matola, Luponde, Itulike, Ramadhani, Kihesa, Utalingolo, Ihalula, Nolle, Mamongoro, Makowo, Ng’elamo, Yakobi, Igominyi, Idunda, Idihani, Lugenge na Kiyaula wameamua kujikita katika suala zima la elimu kwa shule za awali, msingi na sekondari. Majenfo mzuri ya ya kisasa yako katika hatua mbali mbali. Ombi lao ni waalimu wa kutosha.
2. Afya: Ili kuimarisha afya wananchi hao wako katika mpango wa kuwa na zahanati katika kila kata. Tayari kwa kujitolea wameanza ujenzi wa zahanati hizo. Ombi lao ni kupatiwa wauguzi wa kutosha.
3. Kilimo: kutokana na hali ya hewa nzuri ya nyanda za juu kusini, wananjombe hawa wamejizatiti katika kilimo cha chai, mahindi, viazi mviringo na misitu ya mbao.
4. Miundombinu: kwa sehemu kubwa wananjombe wamejitahidi sana kutengeneza barabara za ndani na wanaamini ni kwa barabara nzuri wataweza kufaidika na fursa zitokanazo na migodi ya machimbo ya chuma na mkaa wa mawe ya Mchuchuma na Liganga
No comments:
Post a Comment