Tuesday, October 18, 2011

Mrembo Rahma Swai afariki dunia

Tunasikitika Kutangaza Kifo cha Aliekuwa Mshiriki wa Miss Dar Inter Collage 2010 ambaye pia ni Miss Mtwara 2011/12 ,Rahma Swai (pichani) kilichotokea usiku wa kuamkia leo huko Mtwara.

Mrembo huyo amepatwa na mauti hayo kutokana na tatizo la shinikizo la damu.
Napenda kutoa pole kwa ndugu ,jamaa na marafaiki zake wa karibu na warembo wengine waliomfahamu tangu enzi za uhai wake mpaka mauti yalipomkuta.

Mpango wa Kusafirisha Mwili wa Marehemu kutoka Mkoani Mtwara na kuja jijini Dar es Salaam kwa Mazishi unafanywa na msiba upo nyumbani kwa Bibi yake na Marehemu maeneo ya Makongo,Changanyikeni.

Mungu aiweke mahali pema roho ya Marehemu Rahma Swai

Amein.

Angel Msangi
Mtaribu wa Miss Dar Inter Collage.

No comments: