Mjane wa marehemu Ameria Galinoma ameueleza mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kuwa ratiba ya mazishi itaanza mida ya saa 7 mchana kwa ibada itakayofanyika katika kanisa la RC Tosamaganga na baada ya hapo mwili utasafirishwa hadi makabuli ya Igawa Kalenga kwa mazishi .
Hata hivyo walisema hadi sasa bado hawajapata taarifa ya mgeni atakayeongoza mazishi hayo japo tayari viongozi mbali mbali wa chama na serikali ngazi ya wilaya hadi mkoa wamepata kufika kutoa mkono wa pole.
Mtandao huu umemtafuta mkuu wa mkoa wa Iringa Dr.Christina Ishengoma (MB) ili kujua kama ofisi yake tayari imepata taarifa ya kiongozi yeyote wa kitaifa atakayefika kushiriki mazishi hayo ,amedai bado na kuwa iwapo atapokea taarifa ataujulisha mtandao huu na kuongeza kuwa kwa upande wake atashiriki mazishi hayo .
Habari kwa Hisani ya Freancis Godwin Blog
No comments:
Post a Comment