Monday, April 16, 2012

Just in: Muda Mufpi Baada Ya Mwenyekiti wa UVCCM, Mkoa wa Arusha James Millya Kujiunga CHADEMA Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NEC Chama cha Mapinduzi (CCM)Bw.Nape Nnauye Atoa Tamko Nakusema......!






 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NEC Chama cha Mapinduzi (CCM)Bw.Nape Nnauye(Pichani) ametoa tamko muda mfupi baada ya Mwenyekiti wa UVCCM, Mkoa wa Arusha James Millya kujiunga na CHADEMA na Kusema '' Nampongeza Millya kwa kuamua kukisaidia Chama Changu, kwani alishakuwa mzigo mkubwa kwa CCM.Itakumbukwa alikuwa afukuzwe kwenye chama kutokana na mambo alokuwa akifanya. Akapewa KARIPIO ili apate muda wa kurekebisha tabia yake! Kaondoka akiwa chini ya karipio. Kajivua gamba,tunampongeza kwa kuitikia wito wa kujivua gamba. Kila lakheri aendako ni kijana bado anayo mengi ya kujifunza!''

1 comment:

Castor said...

Nilitegemea Nape, angeanza kwa kujibu hoja alizotoa Millya ktk kujiuzulu kwake.