Sunday, April 15, 2012

ORODHA YA WALIOTEULIWA KUGOMBEA UBUNGE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI




(Inatolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 5(3) ya Nyongeza ya Pili ya Kanuni za Bunge Toleo la 2007)
_______________________________
1.0 Tarehe 9 Machi, 2012 nilitoa Tangazo kwa vyombo
vya habari na gazeti la Serikali juu ya kuwepo kwa nafasi Tisa wazi za Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki kufuatia kufikia ukomo wa maisha ya Bunge la sasa hapo 04 Juni, 2012.
Katika Tangazo hilo niliwaomba wananchi wenye sifa za kugombea nafasi hizo wafanye mchakato wa kugombea kupitia vyama vyao vya Siasa na fomu za wagombea waliopendekezwa zirejeshwe Ofisi ya Bunge kabla ya saa 10.00 jioni tarehe 10 Aprili, 2012 ambayo ndiyo siku ya uteuzi. Jumla ya Wagombea 34 kutoka Vyama vya Siasa vya CCM, CHADEMA, CUF, NCCR-MAGEUZI, TLP, UDP na TADEA wamerudisha Fomu.
2.0 Zoezi la uteuzi limekamilika, Wajumbe 33 wametimiza masharti ya uchaguzi kwa mujibu wa Mkataba wa kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kanuni za Bunge, hivyo, wameteuliwa kugombea nafasi hizo. Aidha, Mgombea mmoja hakutimiza masharti ya uchaguzi ya kuthibitisha uraia wake na kulipa ada ya uchaguzi kwa mujibu wa Kanuni 5(3) na 6 ya Nyongeza ya Tatu ya Kanuni za Bunge, hivyo hakuteuliwa kugombea.

Ifuatayo ni Orodha ya Wagombea walioteuliwa na wasioteuliwa kugombea nafasi za Ubunge wa Afrika Mashariki:-

1. WAGOMBEA WALIOTEULIWA
KUNDI A: WAGOMBEA WANAWAKE
S/NO.
JINA
CHAMA
1.
Nd. Angela Charles Kizigha
CCM
2.
Nd. Fancy Haji Nkuhi
CCM
3.
Dkt. Godbertha Kokubanza Kinyondo
CCM
4.
Nd. Janet Deo Mmari
CCM
5.
Nd. Janet Zebedayo Mbene
CCM
6.
Nd. Maryam Ussi Yahya
CCM
7.
Nd. Rose Daudi Mwalusamba
CUF
8.
Nd. Sebtuu Mohamed Nassor
CCM
9.
Nd. Shy-Rose Sadruddin Bhanji
CCM
10.
Nd. Sofia Ali Rijaal
CCM



KUNDI B: WAGOMBEA WA ZANZIBAR

S/NO.
JINA
CHAMA
1.
Nd. Abdullah Ali Hassan Mwinyi
CCM
2.
Dkt. Ahmada Hamad Khatib
CCM
3.
Dkt. Haji Mwita Haji
CCM
4.
Nd. Khamis Jabir Makame
CCM
5.
Dkt. Said Gharib Bilal
CCM
6.
Nd. Zubeir Ali Maulid
CCM


KUNDI C: WAGOMBEA WA VYAMA VYA UPINZANI

S/NO.
JINA
CHAMA
1.
Nd. Antony Calist Komu
CHADEMA
2.
Dkt. Fortunatus Lwanyantika Masha
UDP
4.
Nd. Juju Martin Danda
NCCR-MAGEUZI
5.
Nd. Micah Elifuraha Mrindoko
TLP
6.
Nd. Mwaiseje S. Polisya
NCCR-MAGEUZI
7.
Nd. Nderakindo Perpetua Kessy
NCCR- MAGEUZI
8.
Nd. Twaha Issa Taslima
CUF








KUNDI D: WAGOMBEA WA TANZANIA BARA


S/NO.
JINA
CHAMA
1.
Nd. Adam Omar Kimbisa
CCM
2.
Nd. Bernard Musomi Murunya
CCM
3.
Nd. Charles Makongoro Nyerere
CCM
4.
Dkt. Edmund Bernard Mndolwa
CCM
5.
Nd. Elibariki Immanuel Kingu
CCM
6.
Dkt. Evans Mujuni Rweikiza
CCM
7.
Nd. John Dunstan Lifa-Chipaka
TADEA
8.
Nd. Mrisho Mashaka Gambo
CCM
9.
Nd. Siraju Juma Kaboyonga
CCM
10.
Nd. William John Malecela
CCM


2. MGOMBEA AMBAYE HAKUTEULIWA

S/NO.
JINA
CHAMA
1.
Nd. Mohamed Abdulrahman Dedes
CUF

3.1 Hivyo, bila ya kuathiri shughuli nyingine zitakazopangwa na Bunge, tarehe 17 Aprili, 2012 saa Nne na nusu asubuhi au muda mfupi baada ya hapo nitawasilisha majina ya Wagombea kwa wapiga kura.

Napenda kutoa shukrani kwa Wagombea wote kwa ushirikiano wao katika kukamilisha zoezi hili la uteuzi. Aidha, tunawaomba wapiga kura, wakati utakapofika, wazingatie matakwa ya Sheria na Kanuni zinazotawala chaguzi hizi.

Imetolewa na:

Dkt. Thomas D. Kashililah KATIBU WA BUNGE NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI
BUNGENI DODOMA
14 APRILI, 2012

No comments: