Saturday, July 30, 2011

NI UNYAMA ULIOJE?...MAITI YA MTOTO MCHANGA YATUPWA JALALANI MBEYA.

Maiti ya mtoto mchanga imekutwa ndani ya mfuko wa Rambo uliotupwa kwenye dampo la shule ya msingi ya Sinde liliyopo kata ya Ruanda mtaa mtoni jijini Mbeya.

Habari za kukutwa kwa maiti ya mtoto mchanga zimetolewa na watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi ambao walikuwa wanaokota mifuko hiyo kwenye dampo hilo kwa ajili ya kwenda kuziuza kwa wafanyabiashara wa mkaa.

Imeeleza kuwa baada ya watoto hao kuifungua Rambo ndipo walipokutana na maiti ya mtoto mchanga na kutoa taarifa kwa wafanyabiashara na wakazi wa mtaa wa Mtoni ambao nao walitoa taarifa kwa jeshi la polisi kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Hata hivyo hakuna mtu anayehisiwa kwenye mtaa huo kuhusika na tukio la kutupwa kwa maiti hiyo, Jeshi la polisi lilifika eneo hilo majira ya saa mbili za usiku na kuondoka na mwili wa mtoto huyo ambaye anadaiwa kuwa na siku moja tangu azaliwe.


No comments: