Saturday, August 13, 2011

BALOZI AMINA SALUM ALI AKUTANA NA MAYOR WA WASHINGTON DC VINCENT GRAY



Alhamisi wiki hii, August 11 2011,Mheshimiwa Balozi Amina Salum Ali na mwakilishi wa Umoja wa Africa nchini Marekani alimtembelea Mayor wa Jiji la Washington DC, Mheshimiwa Vincent Gray. Wawili hao walizungumzia pamoja na mambo mengine, mambo ya usalama na namna ya kupambana na madawa ya kulevya katika jamii, afya huku wakijikita zaidi kwenye masuala ya ukimwi pamoja na namna ya kuboresha biashara kati ya Marekani na bara la Africa. Walikubaliana kimsingi kuwa ofisi hizi zitafanya kazi pamoja katika miradi mbalimbali ikiwemo kulihusisha jiji la Washington DC katika Africa Festival hapo mwaka 2012. Wawekezaji kaeni mkao wa kula.



No comments: