Tuesday, August 16, 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA RASMI MAGHOROFA 30 YA KAMBI YA POLISI BARABARA YA KILWA

Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha, baada ya kuwasili katika viwanja vya maghorofa 30 ya Kambi ya Polisi Barabara ya Kilwa kwa ajili ya kuyazindua rasmi leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua Maghorofa 30 ya Kambi ya Polisi yaliyopo Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam leo Agost 16. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha (kulia) ni Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal akitoa hotuba yake wakati wa kuzindua Maghorofa 30 ya Kambi ya Polisi yaliyopo Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi huo.
Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi huo.
Baadhi ya maofisa wa jeshi la Polisi waliohudhulia hafla hiyo ya uzinduzi, wakisikiliza kwa makini Hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Baadhi ya Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini hotuba wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa msimamizi wa Mradi wa ujenzi wa Maghorofa 30 ya Kambi ya Polisi, Dkt. Huba Nguluma, wakati wa uzinduzi wa majengo hayo uliofanyika leo Agosti 16 Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Kulia kwa Makamu ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha.
Wasanii wa kikundi cha Kwaya cha Polisi, wakitoa burudani wakati wa sherehe za uzinduzi wa maghorofa 30 ya Kambi ya Pilisi Barabara ya Kilwa, yaliyozinduliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, leo Agosti 16. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

No comments: