Na Esther Macha, Mbeya
MAJERUHI 30 waliopata ajali ya Lori waliolazwa katika hospitali teule ya wilaya ya Mbeya Ifisi kati ya 38 waliofikishwa hospitalini hapo juzi baada ya ajali mbaya iliyoua watu 14 wakitokea Mnadani Mbuyuni wilaya ya Chunya mkoani hapa wanaendelea vizuri.
Wakizungumza na mtandao huu jana hospitalini hapo baadhi ya majeruhi hao walisema hali zao kiafya zimeendelea kuimarika baada ya juhudi kubwa za waganga na wauguzi wa hospitali hiyo kuendelea kuwapa matibabu kwa ukaribu kwa kila mmoja wao.
Akizungumza na mtandao huu Mmoja wa majeruhi wa hao Bw.Simon Mwaipopo ambaye amelazwa katika hospitali hiyo, alisema anamshukuru Mungu kwa kunusurika katika ajali hiyo ambapo alitanabaisha kuwa hata waliopona ni kwa uweza wa Mungu pekee.
''Mimi binafsi namshukuru Mungu nimepona na hapa hospitalini tunaendelea kupewa huduma kwa karibu sana na wauguzi pamoja na madaktari jambo ambalo tunaamini baadhi yetu tutapona haraka na kuruhusiwa kurudi nyumbani'' alisema .
Akizungumza na mtandao huu Mmoja wa majeruhi wa hao Bw.Simon Mwaipopo ambaye amelazwa katika hospitali hiyo, alisema anamshukuru Mungu kwa kunusurika katika ajali hiyo ambapo alitanabaisha kuwa hata waliopona ni kwa uweza wa Mungu pekee.
''Mimi binafsi namshukuru Mungu nimepona na hapa hospitalini tunaendelea kupewa huduma kwa karibu sana na wauguzi pamoja na madaktari jambo ambalo tunaamini baadhi yetu tutapona haraka na kuruhusiwa kurudi nyumbani'' alisema .
Majeruhi mwingine Bi.Hilda Jomba ambaye alivunjika mkono wake wa kushoto alisema anaamini atapona baada ya kuendelea kuhudumiwa kwa karibu na wauguzi wa hospitali hiyo bila kumnyanyapaa.
Alisema kuwa wauguzi wanaendelea kuwahudumia vizuri na kwamba katika ajali hiyo anachokumbuka ni kuwa ilikuwa majira ya saa 12 kuelekea kwenye saa moja hivi ndipo walipopinduka na gari walilokuwa wamepanda "alisema .
Kwa upande wake Muuguzi mkuu wa Hospitali hiyo Bi. Rhoda Kasongwa alisema alipokea majeruhi 39 na maiti watatu ambapo maiti wote watatu walitambuliwa na kuchukuliwa na ndugu zao.
Alisema kwa upande wa majeruhi, watatu walipelekwa hospitali ya Rufaa ya Mbeya kwa matibabu zaidi na watatu waliruhusiwa kurejea nyumbani baada ya hali za Afya zao kuimarika.
Muuguzi huyo aliwataja maiti waliofikishwa katika hospitali hiyo na kuchukuliwa na ndugu zao kuwa ni pamoja na Emelia Mwangove (40), Glasiano Kalinga Nyambizi (37) na Msafiri Tinda (35).
Muuguzi huyo aliwataja maiti waliofikishwa katika hospitali hiyo na kuchukuliwa na ndugu zao kuwa ni pamoja na Emelia Mwangove (40), Glasiano Kalinga Nyambizi (37) na Msafiri Tinda (35).
Ajali hiyo ilitokea eneo la Msangamwelu kwa kulihusisha lori aina ya Fuso lenye namba za usajili T 532 AJF na kuthibitishwa na Jeshi la Polisi kupitia kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Bw. Anacletus Malindisa.
Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa polisi Mkoani MBeya Bw.Anacletus Malindisa. alisema kuwa hali za majeruhi waliobaki hospitalini hapo zinaendelea vizuri na ndugu wengine bado wanaendelea kutambua miili ya ndugu zao.
No comments:
Post a Comment