Saturday, February 4, 2012

KIWANDA CHA MAGODOLO CHA PAN AFRICA CHATEKETEA KWA MOTO


Kamanda Misime wa kanda ya kipolisi Wilaya ya Temeke akihojiwa na waandishi wa habari mara baada ya kusimamia zoezi la kuzima moto katika kiwanda cha magodolo cha Pan African kilichopo Chang'ombe jijini Dar es salaam, kiwanda hicho kimeteketea kabisa kwa moto kutokana na mlipuko uliotokea kwenye mashine za kunolea visu vya kukata magodolo kiwandani hapo, Kamanda Misime amesema hakuna taarifa ya mtu yeyote kupoteza maisha wala kujeruhiwa katika tukio hilo la moto

Askari wa vikosi vya kuzima moto wakiwa kazini wakati walipokuwa wakizima moto kiwandani hapo

Magari ya vikosi vya kuzima moto yakiwa yamejipanga katika kiwanda hicho yakiendelea na kazi ya kuzima moto.

Hiki ndiyo kiwanda chenyewe kama kinavyoonekana kikiwa kimeteketea kabisa.

Askari wa kikosi cha kuzima moto wakizima moto huo.

Hawani baadhi raia wa kigeni ambao ni wafanyakzi wa viwanda vya jirani na kiwanda hicho.

Watu mbalimbali wakiangalia tukio hilo.
Picha na John Bukuku wa FULLSHANGWE

No comments: