Friday, March 9, 2012

UWFyamtwaa mama mjasiriamali anayefuata nyayo za mwanamakuka 2012

Pichani shoto ni Meneja matukio na Udhamini wa benki ya NBC,Rachel Remona akimkabidhi Mwanamke Mjasiliamali aliyeibuka na tuzo ya Mwanakuka,Bi.Tatu Mwenda mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni sita.Pichani kati kulia ni Mwenyekiti wa UWF (waandaji wa tuzo hiyo ya Mwanamakuka),Bi.Mwate Madinda sambamba na Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM,Dina Marios wakishuhudia tukio hilo adhimu kabisa,katika kuadhimisha siku ya Mwanamke Duniani,iliyofanyika leo,Hafla hiyo imefanyika usiku huu ndani ya hotel ya Serena,jijini Dar na kuhudhuriwa na watu mbalimbali.
Pichani shoto ni Meneja matukio na Udhamini wa benki ya NBC,Rachel Remona akimkabidhi mshindi wa pili wa tuzo ya Mwanakuka,Bi. Mwanne Msekalile mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni mbili.Pichani kati kulia ni Mwenyekiti wa UWF (waandaji wa tuzo hiyo ya Mwanamakuka),Bi.Mwate Madinda sambamba na Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM,Dina Marios wakishuhudia tukio hilo adhimu kabisa,katika kuadhimisha siku ya Mwanamke Duniani,iliyofanyika leo,Hafla hiyo imefanyika usiku huu ndani ya hotel ya Serena,jijini Dar na kuhudhuriwa na watu mbalimbali
Meneja matukio na Udhamini wa benki ya NBC,Rachel Remona akimkabidhi mshindi wa tatu wa tuzo ya Mwanakuka,Dada Sikudhani Daudi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni moja.
Washindi wa tuzo ya Mwanamakuka wakiwa na mdhamini mkuu pamoja na waandaaji wa tuzo hiyo ya Mwanamakuka.
Mshindi wa tuzo ya mwanamke mjasiriamali ya Mwanamakuka,Bi.Tatu Mwenda akiwa katika picha ya pamoja na wanachama wa UWF huku akiwapungia mkono wageni waalikwa mbalimbali (hawapo pichani) waliofika kwenye hafla hiyo iliyofana kwa kiasi kikubwa.
Mwenyekiti wa UWF,Bi.Mwate Madinda akizungumza machache mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafka hiyo ya tuzo ya Mwanamakuka,kulia kwake ni Meneja Miradi wa UWF,Bi Mariam Shamo.Picha zaidi Bofya Hapa

No comments: