Mgombnea ubunge jimbo la Igunga kupitia CCM, Dkt. Dalaly Kafumu akihutubia maelfu ya wananchi waliofurika kwenye mkutano wa kampeni za chama hicho eneo la Mwanzugi Kata ya Igunga Vijijini, mkoani Tabora, jana.
........................................................
*Mukama asema wana ushaidi, wameripoti polisi
*Mbowe ajibu hizo ni tuhuma za kiongozi dhaifu
*Mnyaa ataka Igunga wakatae CCM wapate maendeleo
Na Waandishi Wetu, Igunga
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. Wilson Mukama amekigeuzia kibao Chama Cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa kimewaingiza Igunga mabaunsa 35 waliopata mafunzo ya kikomandoo nje ya nchi ili kufanya vurugu na kudhuru maisha ya watu.
Madai ya Bw. Mukama ambaye anadai anao ushahidi wa kutosha, yamekuja ikiwa ni siku chache baada ya Chadema kudai kuwa CCM imewapeleka vijana wilayani Igunga na kupata mafunzo ya namna hiyo ili kufanya vujo wilayani humo na kuwatisha wafuasi wa vyama vya upinzani.
Kwa mujibu wa Bw. Mukama makomandoo hao wamesambazwa na Chadema katika kata tano za Igunga na kwamba tayari CCM imeshatoa taarifa kuhusu watu hao katika vyombo vya usalama kwa hatua zaidi, lakini Msemaji wa Polisi katika masuala ya Kampeni, Igunga, Bw. Isaya Mungulu alisema hana taarifa hizo.
Bw. Mukama katika mazungumzo yake na waandishi wa habari alizidi kulia na Chadema akikifananisha na chama cha magaidi cha Renamo cha Msumbiji kilichokuwa msituni kitaka kuchukua madaraka kwa nguvu kwa njia ya mapigano.
Alisema makomandoo hao walipata mafunzo ya ukomandoo katika nchi za za Libya, Israel na Pakstani lakini hakusema imewezekanaje makomandoo kuingizwa wakati kuna vyombo vya ulinzi na usalama.
Alitaja kata ambazo alidai makomandoo hao wamefichwa na idadi yao kwenye mabano kuwa ni Itobo (4), Burede (5), Isakamaliwa (9) Bukene (9) pamoja na Chamacholo (6).
Bw. Mukama alisema hali hiyo inaonyesha kuwa CHADEMA kinataka Tanzania iwe na siasa kama ya nchi zisizo na demokrasia.
Alivitaka vyombo vya habari kuwa waungwana kuandika habari bila upendeleo wala ushabiki na kuonya kuwa kuandika habari zinazoegemea upande wowote ni kudanganya umma.
Alisema CCM inao ushahidi wa barua inayodaiwa kuandikwa na kiongozi mmoja wa Chadema kuonesha kuwa makomandoo hao tayari wapo Igunga na CCM imechunguza na kubaini ni kweli.
Alisema uongozi wa Chadema hauna tofauti na ule wa Kiongozi anayetakiwa kuondoka madarakani nchini Libya, Kanali Muamar Gaddafi wa kuweka watoto wake na jamaa katika madaraka, hivyo Watanzania wasikubali kupigia kura chama hicho.
Kuhusu kampeni za chama hicho, Bw. Mukama alisema zimekwenda kama zilivyopangwa na wanashambulia kama nyuki katika sehemu zote za jimbo hilo na kwamba wananchi wanawaunga mkono na kuahidi kukipigia kura chama chake.
Alisema CCM imeondoa umaskini katika Jimbo la Igunga ambako mwaka 1994 ilikuwa wilaya ya mwisho katika mkoa wa Tabora lakini kwa sasa ni ya kwanza katika sekta mbalimbali.
Mbowe ajibu tuhuma
Akijibu tuhuma hizo, Mwenyekiti wa Chadema, Bw. Freeman Mbowe alieleza kusikitishwa na taarifa ambazo alisema si za kweli.
"Mukama ni mtu ambaye ameingia kwenye siasa uzeeni, Chadema haina kundi lolote iliyofundishwa nje ya nchi wala ndani ya nchi.
Kama Mukama anayo orodha na yeye ni Katibu Mkuu wa chama kinachotawala aweke wazi orodha hiyo ili wakamatwe haraka," alisema Bw. Mbowe.
Alisema chama chake hakijawai kufundisha vijana nchini Israel, Libya, Pakistana wala Afganistan na kwamba hayo ni maneno ya kiongozi dhaifu.
"Hayo ni maneno ya kiongozi mwenye hoja dhaifu ndani ya nchama legelege, chenye kuongoza serikali dhaifu, serikali isiyokuwa na kauli moja," alisema Bw. Mbowe.
Alisema uchaguzi wa Igunga ni mdogo na kwamba vyama mbalimbali ikiwemo Chadema vimepeleka watu kutoka maeneo mbalimbali kusaidia kampeni na kwamba hilo ni jambo la wazi kwa kuwa mji huo umejaa watu kila kona.
"Yeye mwenyewe Mukama ameweka kambi katika Kijiji cha Ulemo zaidi ya watu 400 wamefundishwa na tumelalamika, kama kweli wana ushahidi tumeleta makomandoo kutoka nje wakamatwe haraka, vinginevyo aombe radhi Watanzania," alisisitiza Bw. Mbowe
Alisema kauli hiyo ni udhaifu, unyonge na inaweza kutolewa na mtu ambaye anapiga kelele kutisha umma.
Mnyaa wa CUF ainanga CCM
Mbunge wa Jimbo la Mkanyageni, Kusini Pemba (CUF), Bw. Mohamed Habib Mnyaa amesema kama wananchi wa Jimbo la Igunga wanataka maendeleo ya haraka basi wasikipe kura CCM.
Akimnadi mgombea wa CUF, Bw. Leopold Mahona katika vijiji vya Kata ya Nkinga jana, Bw. Mnyaa pamoja na wabunge wengine zaidi ya 21 kutoka Zanzibar wanaoshiriki kampeni za uchaguzi mdogo alisema jimbo lake la Mkanyageni limepata maendeleo ya maji, umeme na barabara kwa asilimia 70 baada ya kuitakaa CCM.
“Katika Jimbo la Mkanyageni tangu liongozwe na upinzani mwaka 1995 wananchi walikuwa hawajawahi kupata barabara za lami na huduma muhimu za kijamii baada ya kufunguka macho na kubaini kuwa miaka 43 ya uhuru walikuwa wamefungwa na kukaa utumwani mwa CCM walikipigia kura CUF,” alisema Bw. Mnyaa.
Alisema CCM kwa miaka yote tangu Uhuru haijawahi wala kuthubutu kuleta maendeleo yaliyopo, na aliwataka wananchi wa Jimbo la Igunga kumchagua Bw. Mahona kwani atakapoingia bungeni atahakikisha anampa mbinu za kuwaletea maendeleo wananchi wa Igunga.
Bw. Mahona alisema Zanzibar zao lao kuu la biashara la karafuu limekuwa msaada mkubwa kwa wananchi, kwani tangu CUF iingie katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa bei imepanda kutoka sh. 2,500 hadi sh. 12,500 kwa kilo moja.
Aliwaomba wananchi hao ili asaidiane naye kuhakikisha zao la biashara jimbo la Igunga ambalo ni pamba linaimarika na wananchi wafaidike kwa kuuza bei nzuri tofauti na hii iliyopo sasa ya sh. 800 kwa kilo.
Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa CUF, Bw. Hassan Doyo alisema CCM imekuwa ikiomba kura kwa unyeyekevu wakipata madaraka hawakumbuki wananchi wake tena, bali hutumia nafasi hiyo kujilimbikizia mali na rasilimali za wananchi.Chanzo.Majira
*Mbowe ajibu hizo ni tuhuma za kiongozi dhaifu
*Mnyaa ataka Igunga wakatae CCM wapate maendeleo
Na Waandishi Wetu, Igunga
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. Wilson Mukama amekigeuzia kibao Chama Cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa kimewaingiza Igunga mabaunsa 35 waliopata mafunzo ya kikomandoo nje ya nchi ili kufanya vurugu na kudhuru maisha ya watu.
Madai ya Bw. Mukama ambaye anadai anao ushahidi wa kutosha, yamekuja ikiwa ni siku chache baada ya Chadema kudai kuwa CCM imewapeleka vijana wilayani Igunga na kupata mafunzo ya namna hiyo ili kufanya vujo wilayani humo na kuwatisha wafuasi wa vyama vya upinzani.
Kwa mujibu wa Bw. Mukama makomandoo hao wamesambazwa na Chadema katika kata tano za Igunga na kwamba tayari CCM imeshatoa taarifa kuhusu watu hao katika vyombo vya usalama kwa hatua zaidi, lakini Msemaji wa Polisi katika masuala ya Kampeni, Igunga, Bw. Isaya Mungulu alisema hana taarifa hizo.
Bw. Mukama katika mazungumzo yake na waandishi wa habari alizidi kulia na Chadema akikifananisha na chama cha magaidi cha Renamo cha Msumbiji kilichokuwa msituni kitaka kuchukua madaraka kwa nguvu kwa njia ya mapigano.
Alisema makomandoo hao walipata mafunzo ya ukomandoo katika nchi za za Libya, Israel na Pakstani lakini hakusema imewezekanaje makomandoo kuingizwa wakati kuna vyombo vya ulinzi na usalama.
Alitaja kata ambazo alidai makomandoo hao wamefichwa na idadi yao kwenye mabano kuwa ni Itobo (4), Burede (5), Isakamaliwa (9) Bukene (9) pamoja na Chamacholo (6).
Bw. Mukama alisema hali hiyo inaonyesha kuwa CHADEMA kinataka Tanzania iwe na siasa kama ya nchi zisizo na demokrasia.
Alivitaka vyombo vya habari kuwa waungwana kuandika habari bila upendeleo wala ushabiki na kuonya kuwa kuandika habari zinazoegemea upande wowote ni kudanganya umma.
Alisema CCM inao ushahidi wa barua inayodaiwa kuandikwa na kiongozi mmoja wa Chadema kuonesha kuwa makomandoo hao tayari wapo Igunga na CCM imechunguza na kubaini ni kweli.
Alisema uongozi wa Chadema hauna tofauti na ule wa Kiongozi anayetakiwa kuondoka madarakani nchini Libya, Kanali Muamar Gaddafi wa kuweka watoto wake na jamaa katika madaraka, hivyo Watanzania wasikubali kupigia kura chama hicho.
Kuhusu kampeni za chama hicho, Bw. Mukama alisema zimekwenda kama zilivyopangwa na wanashambulia kama nyuki katika sehemu zote za jimbo hilo na kwamba wananchi wanawaunga mkono na kuahidi kukipigia kura chama chake.
Alisema CCM imeondoa umaskini katika Jimbo la Igunga ambako mwaka 1994 ilikuwa wilaya ya mwisho katika mkoa wa Tabora lakini kwa sasa ni ya kwanza katika sekta mbalimbali.
Mbowe ajibu tuhuma
Akijibu tuhuma hizo, Mwenyekiti wa Chadema, Bw. Freeman Mbowe alieleza kusikitishwa na taarifa ambazo alisema si za kweli.
"Mukama ni mtu ambaye ameingia kwenye siasa uzeeni, Chadema haina kundi lolote iliyofundishwa nje ya nchi wala ndani ya nchi.
Kama Mukama anayo orodha na yeye ni Katibu Mkuu wa chama kinachotawala aweke wazi orodha hiyo ili wakamatwe haraka," alisema Bw. Mbowe.
Alisema chama chake hakijawai kufundisha vijana nchini Israel, Libya, Pakistana wala Afganistan na kwamba hayo ni maneno ya kiongozi dhaifu.
"Hayo ni maneno ya kiongozi mwenye hoja dhaifu ndani ya nchama legelege, chenye kuongoza serikali dhaifu, serikali isiyokuwa na kauli moja," alisema Bw. Mbowe.
Alisema uchaguzi wa Igunga ni mdogo na kwamba vyama mbalimbali ikiwemo Chadema vimepeleka watu kutoka maeneo mbalimbali kusaidia kampeni na kwamba hilo ni jambo la wazi kwa kuwa mji huo umejaa watu kila kona.
"Yeye mwenyewe Mukama ameweka kambi katika Kijiji cha Ulemo zaidi ya watu 400 wamefundishwa na tumelalamika, kama kweli wana ushahidi tumeleta makomandoo kutoka nje wakamatwe haraka, vinginevyo aombe radhi Watanzania," alisisitiza Bw. Mbowe
Alisema kauli hiyo ni udhaifu, unyonge na inaweza kutolewa na mtu ambaye anapiga kelele kutisha umma.
Mnyaa wa CUF ainanga CCM
Mbunge wa Jimbo la Mkanyageni, Kusini Pemba (CUF), Bw. Mohamed Habib Mnyaa amesema kama wananchi wa Jimbo la Igunga wanataka maendeleo ya haraka basi wasikipe kura CCM.
Akimnadi mgombea wa CUF, Bw. Leopold Mahona katika vijiji vya Kata ya Nkinga jana, Bw. Mnyaa pamoja na wabunge wengine zaidi ya 21 kutoka Zanzibar wanaoshiriki kampeni za uchaguzi mdogo alisema jimbo lake la Mkanyageni limepata maendeleo ya maji, umeme na barabara kwa asilimia 70 baada ya kuitakaa CCM.
“Katika Jimbo la Mkanyageni tangu liongozwe na upinzani mwaka 1995 wananchi walikuwa hawajawahi kupata barabara za lami na huduma muhimu za kijamii baada ya kufunguka macho na kubaini kuwa miaka 43 ya uhuru walikuwa wamefungwa na kukaa utumwani mwa CCM walikipigia kura CUF,” alisema Bw. Mnyaa.
Alisema CCM kwa miaka yote tangu Uhuru haijawahi wala kuthubutu kuleta maendeleo yaliyopo, na aliwataka wananchi wa Jimbo la Igunga kumchagua Bw. Mahona kwani atakapoingia bungeni atahakikisha anampa mbinu za kuwaletea maendeleo wananchi wa Igunga.
Bw. Mahona alisema Zanzibar zao lao kuu la biashara la karafuu limekuwa msaada mkubwa kwa wananchi, kwani tangu CUF iingie katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa bei imepanda kutoka sh. 2,500 hadi sh. 12,500 kwa kilo moja.
Aliwaomba wananchi hao ili asaidiane naye kuhakikisha zao la biashara jimbo la Igunga ambalo ni pamba linaimarika na wananchi wafaidike kwa kuuza bei nzuri tofauti na hii iliyopo sasa ya sh. 800 kwa kilo.
Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa CUF, Bw. Hassan Doyo alisema CCM imekuwa ikiomba kura kwa unyeyekevu wakipata madaraka hawakumbuki wananchi wake tena, bali hutumia nafasi hiyo kujilimbikizia mali na rasilimali za wananchi.Chanzo.Majira

No comments:
Post a Comment