Sunday, September 11, 2011

Rais Dkt. Jakaya Kikwete awafariji wahanga wa ajali ya Meli Zanzibar

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakimfariji mtoto Said Gerald aliyelazwa katika hospitali ya Mnazi mmoja Zanzibar baada ya kunusurika katika ajali ya meli iliyotokea Unguja juzi usiku.Aliyempakata mtoto Said ni mama yake mdogo Mariam Hemed.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(watatu kushoto) akiwa pamoja na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein(wane kushoto),Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Seif Shariff Hamad(kulia), Waziri wan chi ofisi ya makamu wa kwanza wa Rais anayeshughulikia maafa na muungano, Mohamed Abood Mohamed pamoja Rais Mstaafu wa Zanzibar Amani Abeid Karume wakiwa katika viwanja vya Maisara Unguja kukagua shuguli za kushugulikia miili iliyoopolewa pamoja na kuwafariji wafiwa baada ya kuzama kwa meli huko Unguja juzi usiku
(picha na Freddy Maro).

No comments: