Tuesday, December 13, 2011

WAZIRI MKUU ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA KWENYE Maonesho ya miaka 50 ya Uhuru Jijini Dar es salaam

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bi Joyce Mapunjo na Naibu wake Dkt Shaaban Mwinjaka, wakimpokea Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda kutembelea Banda la Wizara ya Viwanda na Biashara katika siku ya mwisho ya Maonesho ya miaka 50 ya Uhuru Jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Viwanda katika Wizara ya Viwanda na Biashara Bi. Eline Sikazwe akimueleza Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda mafanikio mbali mbali yaliyofikiwa katika Idara yake.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bi Joyce Mapunjo akimpa maelezo Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda juu ya hatua mbali mbali za mafanikio zilizofikiwa na Wizara yake kwa kipindi cha miaka 50 ya Uhuru.
Piki piki ya miguu mitatu (Bajaj) iliyoongezewa ubunifu na kuifanya iweze kutoa huduma ya kusafirisha wagonjwa. Pichani ni mbunifu wa “Ambulance” hiyo Bwana Ally Dahally akionesha ubunifu wake.
Picha ya pamoja ya Wafanyakazi wa Wizara ya Viwanda na Biashara na Taasisi zilizo chini yake mara baada ya kufungwa kwa maonesho ya miaka 50 ya katika Viwanja vya Mwl J.K.Nyerere. Banda la Wizara ya Viwanda na Biashara limekuwa kivutio kikubwa kwa wageni kutokana na maandalizi mazuri na bidhaa mbali mbali zinazozalishwa na Viwanda vya Tanzania.

No comments: