Wednesday, January 4, 2012

Tamko la wanachama wa CUF Dar kuhusu hali ya chama chao



CUF – CHAMA CHA WANANCHI
TAMKO LA WANACHAMA WA CUF MKOA WA DAR ES SALAAM JUU HALI YA KISIASA NDANI YA CHAMA.
Sisi wanachama mkoa wa Dsm,baada ya kuona hali mbaya ya kisiasa ndani ya chama na mwelekeo wa kunyongwa kwa Demokrasia ambapo maamuzi kandamizi yamejitokeza na yanatarijiwa kufanyika katika vikao vinavyoendelea hivi sasa ambavyo mazingira ya kuitishwa kwake vinaashiria dhulma zidi ya haki na utekelezaji wa matakwa ya mtu binafsi, ambapo viongozi wakuu wanaolalamikiwa hawakotayari kukosolewa badalayake wanatumia mamlaka waliyonayo kutoa maamuzi kandamizi.
Sisi kama wanachama na wapenda haki tungependa HAKI SAWA KWA WOTE ionekane ikitendeka na sio kutajwa kinadharia.
Kutokana na hali hiyo tumeona kubainisha madhaifu yaliyopo na madai yetu ya msingi tukitaraji Uziwi na Ukaidi wa Viongozi wetu utakoma hatimae Chama kuleta mvuto mpya:
A: MADAI YA MABADILIKO YA KATIBA
1. Uwepo wa Makamu mwenyekiti bara
2. Mwenyekiti Taifa na Makamu wake wawili waingie kwenye Kamati Tendaji Taifa
3. Pasiwepo ubaguzi katika uwakilishi wa wajumbe wa Wilaya wanaounda Mkutano Mkuu wa Taifa ambapo ukiondoa wajumbe wanaoingia kwa nyadhifa zao ambao Zanzibar pia uzidi, wajumbe 20 wanatoka kila Wila ya Zanzibar wakati Tanzania Bara inatoa mjumbe mmoja tu.
4. Pawepo mabadiliko katika uwakilishi wa Wajumbe wa Balaza Kuu ambapo kwa sasa ,Wajumbe 25 wanatoka Katika Wilaya 123 za Bara na Wajumbe 20 Wanatoka katika Wilaya 10 za Zanzibar.Tofauti hii ya uwiyano na ugumu wa kuhudhuria vikaoni wajumbe wanaotoka TZ Bara kutokana ubovu wa miundombinu na umbali wa maeneo wanakotoka unatoa mwanya kwa Katibu mkuu kuitisha vikao kandamizi vyenye kupitisha matakwa binafsi ya Sefu Sharif na mfumo wa upendeleo wa Wapemba
5. Mfumo wa uteuzi wa viti maalum ubadilishwe kwa kuwa unaua bara , kutokana na kuzidi kujaza wabuge Zanzibar badala TZ Bara penye hitajio kubwa la wabunge wasaidie kujenga Chama na ikizingatiwa nafasi hizo ni hesabu ya kura tulizopigania watu wa Bara kwani Zanzibar kurazao ni chache.
6. Kuendelea kwa Chama kuitumia katiba ya zamani ya toleo la 2003 wakati mkutano mkuu wa taifa wa 2010 LAND MARCK HOTEL ulipitisha katiba iliyo na vipengele vipya haitumiki mpaka hii leo ni kuvunja sheria na ushahidi wa dharau kwa wajumbe wa mkutano mkuu na wanachama matawini.
B: UTAWALA NA UTENDAJI
1. Mwenyekiti Taifa hana ofisi zanzibar wakati katibu Mkuu na makamu Mweyekiti wana ofisi Makao makuu Zanzibar na ofisi kuu bara.
2. Asilimia zaidi ya 80 ya ajira za madereva na wafanyakazi wengine wa ofisi kuu bara wanatoka zanzibar wakati hakuna madereva wanaofanya kazi zanzibar wanaotoka Bara.
3. Kuna matatizo ya mgawanyo wa raslimali za chama kati ya Bara na Zanzibar,mifano mgao wa Chama wa bajeti ya uchazi mkuu 2010 Zanzibar yenye wilaya 10 katika Mikoa 5 imepewa sh.500 milioni wakati Bara yenye wilaya 123 katika Mikoa 23 imepewa sh.70 milioni tu,fursa za Elimu na Mikopo,magali 5 ya Chama yameuzwa bila ya kufua taratibu za tenda.
C: UDHAIFU WA SEFU
1. Amekua kiongozi hodari wa kufukuza au kusababisha kuhama kwa viongozi hodari wa Tanzania Bara kama:-
(a) Mhe. James Mapalala
(b) Mhe. Maiko Nyaluba
(c) Mhe. Slivesta Kasulumbai
(d) Mhe. Geoge Shambwe
(e) Mhe. Shaibu Akwilombwe
(f) Mhe. Richard Hiza Tambwe
(g) Mhe. Wilfred Lwakatare
(h) Mhe. Othman Dunga
(i) Mhe. Asha Ngende
(j) Mhe. Khamisi Katuga
(k) Mhe. Ashura Amazi
Kwa upande wa Zanzibar ni pamoja na
a.Naila Jilawi
b.Fatuma Magimbi
c.Juma Othuman
d.Salumu Msabaha
Watu wengi waliofukuzwa au kulazimika kuhama Chama ilitokana na mfumo wenye nguvu usio rasmi ndani ya Chama unaomkinga Maalim Sefu asikosolewe
2. Toka kuanzishwa CUF hajafanya ziara au vikao hata mara moja katika mikoa na wilaya nyingi za Tanzania Bora
3. Amekuwa bingwa wa kufanya maamuzi makubwa ndani ya Chama yeye binafsi nje ya katiba na utaratibu wa vikao mfano
Kumtambua Karume na kukiuka maamuzi ya Baraza kuu la Uongozi Taifa
(a).CUF imeambulia mawaziri 7 tu CCM ina mawaziri 9 lakini wakuu wa mikoa, wakuu wilaya na watedaji wote wa serikali ni wa CCM yeye analilridhia.
(b). Ilani ya inayo tekelezwa zanzibar ni ya CCM wakati inadaiwa ni serekali ya umoja wa kitaifa
(c).Ubaguzi wa upemba ndani ya chama.
Nahaya yanayoendelea Chama kumdhibiti Mh.Hamadi Rashidi ni uthibitisho juu ya Maalim Sefu kukiburuza chama anavyotaka
a.Uundwaji wa kamati ya nidhamu na maadili kinyume na katiba ya chama.
b.kamati ya utendaji taifa imewajadili watuhumiwa bila kuwapa nafasi ya kujieleza ambapo ni haki yao kwa mujibu katiba
c.Kamati tendaji inaongozwa na Maalim Sefu akisaidiwa na wengi wa wajumbe wake ambao wameonyesha chuki za dhahiri na tayari wameshawahukumu watuhumiwa nje ya fikao mfano.E nail ya mwenye kiti wa kamati tendaji taifa sefu kwenda kwa mwenyekiti Prof.Lipumba ilishapanga namna ya kuwafukuza watuhumiwa ya 14.decembr 2012
d.Tamko la Naiba katiba mkuu bora julius mtatiro kwa press tarehe 13.12.2011 ofisi kuu buguruni la kuwatangaza watuhumiwa kuwa ni waasi na kuwapa kuwashuhulikia nje ya vikao katiba na taratibu za chama bila kuwapa nafasi ya kujieleza
e.Kauli za N.katibu mkuu Zanzibar Ismail Jusa makamu mwenyekiti Machano khamisi Ali katika maeneo mbalimbali na ofisi kuu kuwa tutawa wafukuza kama kama akina Mapalala
Hamad mwana wa haramu ni mwana wa haram tu,hata ukimuweka ndani ya chupa atatoa kidole nje ili aone kama!! Ambayo ni kashfa
c.Matumizi ya vitisho dhidi ya watuhumiwa yanadhihirisha kuwa wasioweza kutenda haki.
d.Kikao kilicho fanyika zanzibar cha kamati Tendaji ya Taifa inadhihirishwa kuwa lengo lake lilikuwa ni ubaguzi ilikikao kikifanyika yeye akawa hayupo basi kikao hicho kitaongozwa na Jusa Ismaili ambaye alisha watukana
Blue Guard Bara akiwemo mzee Juma wandwi kwamba wao ni mbwa wanatumiwa na watu wa Zanzibar katika ukumbi wa Diamond Tubilie,mwaka 2009 wakati wa mkutano mkuu
Baraza kuu limehitimishwa tarehe 4/01/2012 lina fanyika Zanzibar baada ya kikao cha kamati tendaji taifa tarehe 30 na 31 /12/2011 kutokana na mgawanyiko wa kijiografia wa wajumbe wa Baraza KuuTanzania
Baraza na hali ya miundo mbinu, Wajumbe wengi toka Tanzania Bara watashindwa kuhudhuria na hivyo kutoa nafasi ya wajumbe wa Zanzibar wanao muunga mkono sefu kufanya maamuzi kandamizi dhidi ya agenda za Tanzania bora
TAMKO LA WANACHAMA.
Sisi wanachama, tuliokutana
Leo tarehe 1. 1. 2012 tuta hamasisha wanachama miko yote na hasa Tanzania Bara kuandamana kuelekea ofisi kuu ya CUF Buguruni kupinga mipango haramu ya kufukuzwa kwa wanachama wenzetu nje ya utaratibu wa kikatiba,
Tutachukua hatua za kisheria dhidi ya viongopzi wote wanao kiuka katiba halali ya chama.
Tunatoa rai kwa baraza kuu la uongozi Taifa kulimaliza suala hili kwa njia za kusuhulishana ndani ya vikao bila kufukuzana kwa njia zilezile zilizo tumika kukaa na wauji wa CCM serekali yake waliona wanachama wa CUF Bara na visiwani katika maandamano ya januari,26 na 27 na 2001 kuliko hatua wanazo tarajia kuzichukua za kufukuzana.
................................................. …………………………………….
Mwenyekiti Kamati ya Dharura Katibu Kamati ya Dharura
Hamdan Ngulangwa (0715 552699) Mpenda I. Mpenda (0715 664913)
……………………………………
Mweka Hazina kamati ya dharura
Leyla Husein (0719 827047)
Kutoka jamiiforums

No comments: