Friday, January 20, 2012

Turkish Airline Tanzania yaendesha warsha ya siku moja iliyokutanisha makampuni ya mawakala wa kuuza tiketi za ndege

Mwenyekiti wa Baraza la Maendeleo ya Utalii na afya Uturuki (Turkish Hearth careand Tourism Development),Bw. Emim Cakmak akizungumza katika warsha ya siku moja iliyokutanisha makampuni ya mawakala wa kuuza tiketi za ndege na baadhi ya viongozi wa dini ya Kikristo, Warsha hiyo ilikuwa ikizungumzia maeneo mbalimbali yenye historia ya Ukristo ambayo wakristo wanaweza kutembelea na kujionea kumbukumbu hizo na imefanyika leo katika hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam jijini Dar es salaam
Meneja wa Turkish Airline Tanzania,Bw. Mustafa Ozkahraman akitoa mada katika warsha hiyo juu ya mambo mbalimbali na ubora wa huduma za usafiri wa anga wa shirika hilo, kushoto ni Bw. Emim Cakmak Mwenyekiti wa Baraza la Maendeleo ya Utalii na afya Uturuki. (Turkish Hearth careand Tourism Development)
Wadau mbalimbali wakiwa katika warsha hiyo kwenye hoteli ya Hyyat Regency Dar es salaam leo.
Baadhi ya masista pia wamehudhuria katika warsha hiyo iliyoandaliwa na shirika la ndege la Turkish Airlines.
Kutoka kushoto ni )Bw. Emim Cakmak Mwenyekiti wa Baraza la Maendeleo ya Utalii na afya Uturuki(Turkish Hearth careand Tourism Development), Mustafa Ozkahraman Meneja wa Turkishh Airline Tanzania na Victoria Carmak Meneja Huduma wa Hello Tourism Travel Agency wakiwa katika picha ya pamoja leo.
Baadhi ya viongozi wa dini madhehebu ya Kikristo wakiwa katika warsha hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya Hyyat Regency jijini Dar es salaam leo.

No comments: